
Hii ni riwaya inayozungumzia maisha ya kijana aitwaye Utubora. Kama jina lake lilivyo, kijana huyu anajipambanua kuwa ni mtu jasiri, imara, mvumilivu, mwaminifu, mkweli na mwenye misimamo imara katika maamuzi yake. Mwandishi amemchora mhusika huyu kama kielelezo cha vijana wengi wanaokumbana na misukosuko mingi na mibaya kama siyo michungu katika maisha yao.
Kwanza kabisa kijana huyu anashindwa kuendelea na maisha ya masomo baada ya baba yake kufariki ghafla. Mungu hamtupi mja wake. Utubora anapata kazi ya ukarani katika kampuni ya tajiri Ahmed. Hapa Utubora anakuwa maarufu kuliko watu wote kwenye ofisi ya karafuu na matokeo yake analipwa mshahara mkubwa na kuwa gumzo Unguja nzima.
This book is categorised in
No reviews , Be the first to write a review
- ISBN : 9789976583816
- Publication Date : June 2023
- Language : Swahili
- Number of Pages : 97
- Cover Format : Softcover
- Edition : First Edition