
Dhifa ni diwani ya mwisho ya Kezilahabi. Diwani hii inakusanya tungo za miaka ya 1990-2008, wakati wa mageuzi ya kiliberali mamboleo yaliyoasisiwa na Rais Ali Hassan Mwinyi na kuendelezwa na warithi wake baada ya Mwalimu J.K. Nyerere kustaafu. Jina la diwani linaakisi wazo lake kuu: “Dhifa” – yaani sherehe ya kujinufaisha baada ubinafsishaji na uporaji wa mali na rasilimali za Umma. Jina la diwani hii linabeba motifu kuu ya kipindi hicho: ufisadi na ubadhirifu uliokithiri.
- ISBN : 9789976587074
- Tarehe ya kuchapishwa : October 2022
- Lugha : Swahili
- Idadi ya kurasa : 67
- Aina ya kava : Softcover
- Toleo : First Edition
Jamii ya kitabu hiki ni
Hakuna maoni , Kuwa wa kwanza kuandika maoni