Dunia Uwanja wa Fujo
Paperback

“Dunia uwanja wa fujo” inaelezea jinsi maisha yaliyopo duniani ni sawa sawa na fujo kwani kila mtu anayekuja duniani huleta fujo zake na baadae kutoweka. Mwandishi E. Kezilahabi anaelezea katika jamii kila mtu anakuja duniani kufanya fujo zake na kusababisha matatizo mbalimbali katika jamii yake kama vile mauaji, ukabila, umalaya, uchawi, ubakaji ulevi wa kupindukia nk. hivyo basi mwandishi anaamini kwamba katika dunia kila mtu anakuja na fujo zake na kutoweka, mfano mhusika Tumaini katika Riwaya hii ameleta fujo zake kama vile umalaya,  mauaji na mengine mengi na baadae kutoweka.

Euphrase Kezilahabi

Euphrase Kezilahabi alizaliwa Namagondo, Ukerewe, Tanzania, tarehe 13/4/1944. Alisomea katika seminari ya Nyegezi, Mwanza (1957-66) na baadaye Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, alikohitimu mwaka 1970. Alihitimu digrii ya Uzamivu katika Fasihi katika Chuo Kikuu cha Wisconsin, Madison, Marekani, mwaka 1985. Alikuwa Mhadhiri na baadaye Profesa Mshiriki katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam na baadaye Chuo Kikuu cha Botswana hadi alipougua mwaka 2019. Kezilahabi alifariki tarehe 9/1/2020 na kuzikwa, Namagondo, Ukerewe tarehe 13/1/2020. Mbali na DHIFA, Kezilahabi ameandika vitabu vingine 9, zikiwamo riwaya 6, tamthiliya 1 na diwani 2 za ushairi. Ameandika pia hadithi fupi nyingi.

Taarifa za kitabu
  • ISBN : 9789976587043
  • Tarehe ya kuchapishwa : January 2023
  • Lugha : Swahili
  • Idadi ya kurasa : 233
  • Aina ya kava : Paperpack

Jamii ya kitabu hiki ni
Maoni kutoka kwa jamii
Na Euphrase Kezilahabi